LINDI-Timu ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments (WHI) imeendelea na ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa nyumba za Watumishi katika Mkoa wa Lindi ambapo Juni 27, 2026 imekagua maendeleo ya ujenzi wa nyumba za Watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Shule ya Sekondari Matanda, Shule ya Msingi Runyu, Kituo cha Afya Mvuleni na Shule ya Sekondari Mvuleni.
Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ikikagua ubora wa kazi za ujenzi wa nyumba ya watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi tarehe 27 Juni 2026.
Timu ya wataalamu kutoka Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ikikagua ubora wa kazi za ujenzi wa nyumba ya watumishi katika Kituo cha Afya Hoteli Tatu, Wilaya ya Kilwa, Mkoani Lindi tarehe 27 Juni 2026.
Timu ya wataalam kutoka Ofisi ya Rais-UTUMISHI na Utawala Bora na Watumishi Housing Investments ikiongozwa na Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute kukagua mradi wa maendeleo wa ujenzi wa Kituo cha Afya Mvuleni kilichopo Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.Muonekano wa mbele wa jengo la mradi wa makazi ya Watumishi wa Umma wa shule ya sekondari Mvuleni kwenye Halmashauri ya Manispaa ya Lindi, mkoa wa Lindi.
Mkurugenzi wa Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Bw. Patrick Allute akijadili jambo na Wataalamu kutoka Ofisi hiyo na Watumishi Housing Investments (WHI) mara baada ya kukagua utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za Watumishi wa Shule ya Sekondari Mvuleni iliyopo katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi,Mkoa wa Lindi.

.jpeg)
.jpeg)
