Wananchi waendelea kuchota maarifa banda la Wizara ya Fedha katika Wiki ya Utumishi wa Umma jijini Dodoma

DODOMA-Wizara ya Fedha imeungana na Wizara, Taasisi za umma pamoja na Sekta binafsi, kushiriki katika Maonesho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kutoa elimu kwa wananchi kuhusu majukumu ya Wizara katika usimamizi wa fedha za umma, ukuaji wa uchumi wa Taifa na utekelezaji wa mipango ya maendeleo.
Maonesho hayo yenye kauli mbiu “Kuchochea uwajibikaji jumuishi kwa maendeleo endelevu”, yanafanyika katika Viwanja vya Chinangali, jijini Dodoma kuanzia tarehe 16-23 Juni, 2026.
Wizara ya Fedha inawakaribisha wananchi wote kutembelea Banda la Wizara ya Fedha, ili kupata elimu, taarifa na huduma mbalimbali zinazotolewa na Wizara pamoja na taasisi zake, sambamba na kujionea mafanikio na maboresho yanayoendelea kutekelezwa katika sekta ya fedha na uchumi nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here