Balozi Nyamanga aongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 121 wa Baraza la Mawaziri wa OACPS

BRUSSELS-Balozi wa Tanzania nchini Ubelgiji, Mhe. Jestas Abuok Nyamanga, kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.), ameongoza Ujumbe wa Tanzania katika Mkutano wa 121 wa Baraza la Mawaziri wa OACPS uliofanyika Brussels, Ubelgiji, tarehe 15–16 Julai 2026.
Mkutano huo umejadili na kukubaliana kuhusu hatua za utekelezaji wa Maazimio ya Mkutano wa 11 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa OACPS uliofanyika Malabo, Equatorial Guinea, mwezi Machi 2026.
Maeneo yaliyopewa kipaumbele katika utekelezaji wa maazimio hayo ni pamoja na kuendeleza uchumi wa buluu, kuimarisha biashara na uwekezaji, kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, kuharakisha mageuzi ya kidijitali, kuimarisha minyororo ya thamani, na kukuza ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo baina ya Nchi Wanachama 79 wa OACPS kutoka Afrika, Karibiani na Pasifiki.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here