BoT Sabasaba yaendelea kuwaleta pamoja viongozi na wananchi kupata elimu na kujionea huduma mbalimbali

DAR-Viongozi mbalimbali wameendelea kutembelea banda la Benki Kuu ya Tanzania (BoT) katika Maonesho ya 50 ya Biashara ya Kimataifa (Saba Saba) yanayoendelea katika Viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere, Barabara ya Kilwa, jijini Dar es Salaam.
Miongoni mwa viongozi waliotembelea banda hilo ni Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Laurent Luswetula, pamoja na Katibu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Baraka Leonard.

Wakati wa ziara zao, viongozi hao walipata fursa ya kujionea huduma mbalimbali zinazotolewa na wataalamu wa BoT, pamoja na kupata elimu kuhusu majukumu yake katika kusimamia sera ya fedha, kudumisha utulivu wa mfumo wa fedha na kuchochea maendeleo endelevu ya uchumi nchini.
Benki Kuu inaendelea kuwakaribisha wananchi kutembelea banda lake ili kupata elimu na kufahamu kwa undani zaidi kuhusu majukumu yake, huduma na mchango wake katika maendeleo ya uchumi wa Taifa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here