Kampeni ya Chagua Ndoto,Kataa Dawa za Kulevya ya DCEA yawafikia wanafunzi 10,137 wilayani Tunduma

RUVUMA-Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imewafikia wanafunzi 10,137 kutoka shule 13 za sekondari wilayani Tunduma kupitia kampeni ya “Chagua Ndoto, Kataa Dawa za Kulevya.”
Shule zilizoshiriki katika kampeni hiyo ni Uwanjani Secondary School, Majengo Mjini Secondary School, Twiza Secondary School, Tunduma Secondary School, Mpakani Secondary School, Danida Secondary School, Mwl. Nyerere Secondary School, Mpande Secondary School, Jakaya Kikwete Secondary School, Katete Secondary School, Sumange Secondary School, Mpemba Secondary School na Tunduma Town Council Secondary School.
Kupitia elimu hiyo, wanafunzi wamejengewa uelewa kuhusu madhara ya dawa za kulevya kiafya, kisaikolojia, kielimu na kijamii, namna ya kujikinga dhidi ya matumizi yake, kukabiliana na ushawishi wa makundi hatarishi, kufanya maamuzi sahihi, pamoja na umuhimu wa kutoa taarifa na kutafuta msaada.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here