Taasisi ya Elimu Tanzania (TET) imepongezwa kwa kukamilisha kwa wakati uandishi na uchapaji wa vitabu vya Elimu ya Dini ya Kiislamu (EDK) kwa Kidato cha Sita, hatua inayowezesha wanafunzi kuanza kutumia vitabu hivyo katika utekelezaji wa mtaala mpya wa elimu.












Pongezi hizo zimetolewa na Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Adolf Mkenda, wakati alipokabidhi vitabu hivyo kwa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na Ofisi ya Mufti Mkuu wa Zanzibar katika hafla iliyofanyika Julai 22, 2026, kwenye Ukumbi wa Mfalme Mohammed wa Sita, Makao Makuu ya BAKWATA jijini Dar es Salaam.Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi wa dini, maafisa wa Serikali na wadau mbalimbali wa sekta ya elimu na dini ya Kiislamu.
Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Mkenda alisema Serikali itaendelea kutekeleza Sera ya Elimu kwa kuhakikisha kila mwanafunzi nchini anapata elimu yenye ubora na fursa sawa za kujifunza, bila kujali eneo analotoka au somo analolisoma.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo







