NA DIRAMAKINI
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa Asha Dachi Mbaruk kuwa Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Julai 14, 2026 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka, Mbaruk anachukua nafasi iliyoachwa na Dkt. Ayub Rioba Chacha ambaye amemaliza muda wake wa kulitumikia shirika hilo.
Kabla ya uteuzi huo, Mbaruk alikuwa akihudumu kama Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Magazeti ya Serikali (TSN), nafasi aliyoshikilia kwa kipindi tofauti kabla ya kuhamia TBC.
Tags
Asha Dachi Mbaruk
Dr Samia Suluhu Hassan
Habari
Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC)
TBC Taifa
Uteuzi TBC
