Rais Dkt.Samia apokea Ujumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC)

DAR-Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Julai 19,2026 amepokea Ujumbe Maalum kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mheshimiwa Félix Antoine Tshisekedi, uliowasilishwa na Waziri wa Ushirikiano wa Kikanda Mhe. Floribert Anzuluni Isiloketshi, Ikulu jijini Dar es Salaam.
Pamoja na kupokea Ujumbe huo, Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya mazungumzo na Mhe. Floribert Isiloketshi na kumuahidi kuwa Tanzania itaendeleza na kuimarisha uhusiano na ushirikiano wa muda mrefu na wa kindugu uliopo kati ya Tanzania na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika masuala mbalimbali yenye maslahi kwa nchi zote mbili.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here