DAR-Rais wa Jamhuri ya Kiarabu ya Misri Mheshimiwa Abdel Fattah EL-Sisi, amewasili jijini Dar es Salaam Julai 18,2026, kuanza ziara ya Kitaifa ya siku moja kufuatia mwaliko wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Ziara hii itahusisha mazungumzo kati ya viongozi wa mataifa hayo mawili rafiki, yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia, pamoja na kupanua ushirikiano katika sekta mbalimbali za maendeleo, ikiwemo biashara, uwekezaji, kilimo, nishati, maji, afya, elimu na miundombinu.














