Rais wa TFF ateta na uongozi wa Jiji la Atlanta

ATLANTA-Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia amefanya mazungumzo ya ushirikiano na uongozi wa Jiji la Atlanta, Marekani.
Mazungumzo ya pande hizo mbili yalilenga maeneo ya mpira wa miguu wa wanawake, mpira wa miguu wa vijana, utalii pamoja na ushirikiano kati ya Atlanta na majiji mengine ya Tanzania.
Ziara ya Rais Karia ambaye aliambatana na Marais wa mashirikisho mengine, ilitokana na mwaliko wa Meya wa Jiji la Atlanta, Andre Dickens.
Mbali ya mazungumzo hayo, Rais Karia alipata fursa ya kutembelea Uwanja wa Mercedes- Benz uliopo Atlanta ambao utatumika kwa mechi ya leo ya nusu fainali ya Kombe la Dunia kati ya England na Argentina.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here