DAR-Jeshi la Polisi kupitia Polisi Kata wa Tungi, Wilaya ya Kigamboni mkoani Dar es Salaam, limeendelea kuimarisha juhudi za kulinda haki na usalama wa watoto kwa kutoa elimu kuhusu namna sahihi na rahisi ya kuripoti vitendo vya ukatili vinavyoweza kufanywa dhidi yao.
Elimu hiyo imetolewa Julai 8,2026 na Polisi Kata wa Tungi, Mkaguzi wa Polisi (INSP) Diogeness Mganyizi alipokutana na kundi la watoto katika programu ya uelimishaji iliyolenga kuwajengea uelewa kuhusu haki zao pamoja na umuhimu wa kutoa taarifa mapema wanapokumbana na vitendo vya ukatili.


