Wizara ya Madini yaahidi kushirikiana na UAIT kukuza uongezaji thamani madini ya Vito

DODOMA-Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Madini, Msafiri Mbibo amekihakikishia ushirikiano Chuo cha United African Institute of Technology (UAIT) Cha Korea Kusini katika kuendeleza mafunzo ya uongezaji thamani madini ya vito kupitia Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC).
Ahadi hiyo imetolewa Julai 9,2026 jijini Dodoma, wakati wa kikao kati ya Naibu Katibu Mkuu na Mkuu wa Chuo cha UAIT, Prof. Chang Ki Lee.
Akizungumza katika kikao hicho, Mbibo amesema ushirikiano huo utaiwezesha Tanzania kuzalisha wataalamu wengi wazawa wenye ujuzi wa kiwango cha juu katika shughuli za uongezaji thamani wa madini ya vito, hatua itakayochangia kuongeza thamani ya rasilimali za madini na kukuza uchumi wa nchi.

Aidha, viongozi hao wamejadiliana fursa mbalimbali za kuimarisha ushirikiano katika maendeleo ya Sekta ya Madini, mafunzo ya kitaalamu na matumizi ya teknolojia za kisasa ili kuongeza ushindani wa sekta hiyo nchini.
Kituo cha TGC kilichopo jijini Arusha, kinatoa mafunzo ya ngazi mbalimbali kwa muda mrefu na mfupi ya uongezaji thamani madini ya vito.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here