Magazeti leo Agosti 16,2026

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Agosti 14, 2026 imepitia na kuujadili mkakati wa kuimarisha huduma za Maji, lishe, upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira kwenye shule za msingi na Sekondari nchini, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kuelekea Mkutano wa Nne wa Bunge unaotarajiwa kuanza Agosti 25, 2026.
Katika kikao hicho, Kamati imejadili kwa kina namna bora ya uimarishaji wa huduma za maji , upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira kwenye Shule za msingi na sekondari nchini, pamoja na uimarishaji wa lishe katika shule za msingi nchini.

Mara baada ya kuupitia mkakati huo, Kamati kupitia Mwenyekiti wake Mhe. Florent Kyombo, katika eneo la lishe imeitaka OWM – TAMISEMI kufanya utafiti wa kina ili kuwa na takwimu halisi za lishe mashuleni, kuimarisha somo la kilimo mashuleni ili kuwapatia ujuzi wa kilimo wanafunzi, ikiwa ni pamoja na kupata chakula cha kutosha mashuleni.









Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here