Mtaalamu katika Sekta ya Mafuta nchini, Dkt. Sajad Habib Rai, amempongeza Makamu wa Rais, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa kuapishwa kushika nafasi hiyo, huku akimtabiria mambo makubwa katika utekelezaji wa majukumu yake ya kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan.



Akizungumza jijini Dar es Salaam, siku moja baada ya uapisho wa Makamu wa Rais huyo uliofanyika Ikulu ya Chamwino, Dodoma, Dkt. Sajad amesema ana imani kubwa na kiongozi huyo, huku akimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uteuzi wa Ndejembi.
Dkt. Sajad, ambaye ni Meneja Mkazi wa Mansoor Industries nchini, amesema hana shaka na uwezo wa Ndejembi katika uongozi, akisisitiza kuwa sifa na uwezo alionao ni nyenzo muhimu katika kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan.
“Kwa kipindi kifupi alichohudumu katika Wizara ya Nishati kwa nafasi ya uwaziri, Mheshimiwa Ndejembi amekuwa mtu muhimu aliyesimama kikamilifu katika kushughulikia masuala mbalimbali. Hii ni sifa ambayo si kila kiongozi anayo,” amesema Dkt. Sajad.










Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo














