Magazeti leo Agosti 31,2026

Mtaalamu katika Sekta ya Mafuta nchini, Dkt. Sajad Habib Rai, amempongeza Makamu wa Rais, Mhe. Deogratius Ndejembi, kwa kuapishwa kushika nafasi hiyo, huku akimtabiria mambo makubwa katika utekelezaji wa majukumu yake ya kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan.
Akizungumza jijini Dar es Salaam, siku moja baada ya uapisho wa Makamu wa Rais huyo uliofanyika Ikulu ya Chamwino, Dodoma, Dkt. Sajad amesema ana imani kubwa na kiongozi huyo, huku akimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa uteuzi wa Ndejembi.

Dkt. Sajad, ambaye ni Meneja Mkazi wa Mansoor Industries nchini, amesema hana shaka na uwezo wa Ndejembi katika uongozi, akisisitiza kuwa sifa na uwezo alionao ni nyenzo muhimu katika kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan.

“Kwa kipindi kifupi alichohudumu katika Wizara ya Nishati kwa nafasi ya uwaziri, Mheshimiwa Ndejembi amekuwa mtu muhimu aliyesimama kikamilifu katika kushughulikia masuala mbalimbali. Hii ni sifa ambayo si kila kiongozi anayo,” amesema Dkt. Sajad.










Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here