Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC) limetoa wito kwa wananchi wa Manispaa ya Kahama hususan wakazi wa Kata ya Mwendakulima kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo katika kituo cha mafunzo ya kilimo kilichopo Kata ya Mwendakulima wilayani Kahama mkoani Shinyanga kilicholenga kuwainua wananchi katika sekta ya kilimo.


Akizungumza baada ya kutembelea kituo hicho, Mkurugenzi wa Uwezeshaji na Ushiriki wa Watanzania, Neema Mwakatobe amesema kuwa, wametembelea kituo hicho na kuona fursa nyingi zinazopatikana katika kituo hicho.
“Tunashukuru kwa mwaliko huu ambao umetufanya tufike hapa,tumetembelea kituo hiki na tumeona fursa mbalimbali zinazopatikana katika kituo hiki ambazo zinaweza kuwainua wananchi kiuchumi,tumeona maeneo yenye changamoto na tumeweka mikakati na manispaa ya Kahama ya kuweza kuimarisha kituo hiki,hivyo wananchi wanatakiwa kuchangamkia fursa kituo hiki,”amesema Mwakatobe.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo













