Magazeti leo Agosti 26,2026

Mkuu wa Chuo cha Uhasibu Arusha (IAA), Prof. Eliamani Sedoyeka amesema IAA itaendelea kuimarisha miundombinu na mazingira ya kujifunzia ili kandaa watalaam mahiri na kuendana na mahitaji ya programu za kisasa hususani programu zinazohusisha matumizi makubwa ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano.
Prof. Sedoyeka amesema hayo katika hafla ya uzinduzi wa utoaji wa programu za Shahada ya Uhasibu na Teknolojia ya Habari (Bachelor Degree in Accountancy with IT) na Shahada ya Sayansi ya Kompyuta (Bachelor Degree in Computer Science) katika Kampasi ya Babati iliyofanyika Waangw’aray Mjini Babati.

“Tunaishukuru Serikali kupitia Mradi wa Elimu ya Juu kwa Mageuzi ya Kiuchumi (HEET) imetoa jumla ya shilingi bilioni 13.7 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala, mkataba na maabara ya TEHAMA katika Kampasi ya Babati. Sisi pia tumewekeza katika teknolojia na mkakati wetu ni madarasa yetu yote yawe smart classes (madarasa janja),” amesema.

Prof. Sedoyeka ameongeza kuwa dhamira ya IAA ni wanafunzi kujifunza katika mazingira yanayowapa nafasi ya kupata maarifa, kufanya mazoezi, kubuni, kujiandaa kwa mahitaji halisi ya dunia ya kazi na kuwa kutumia maarifa kutatua changamoto halisi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here