Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) imeeleza kuwa matumizi ya mifumo ya kidijitali katika vyama vya ushirika yameleta mapinduzi makubwa katika usimamizi wa shughuli za ushirika nchini, huku zaidi ya vyama 6,000 vikisajiliwa kwenye mfumo maalum wa kidijitali.
Meneja wa Mawasiliano wa e-GA, Subira Kaswaga, amesema kuwa mfumo huo umewezesha kuongeza uwazi katika biashara za mazao, kupunguza mianya ya upotevu wa mapato pamoja na kuwapa wakulima uwezo wa kufuatilia mwenendo wa mauzo ya mazao yao kwa wakati.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo














