Magazeti leo Septemba 16,2026

Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) imeendelea kutekeleza shughuli za uthibiti wa ubora wa mbegu nchini kwa kutembelea Mkoa wa Manyara, Wilaya ya Babati, ambapo imefanya ukaguzi katika shamba lenye ukubwa wa ekari 25 linalozalisha mbegu za vitunguu aina ya Mang’ola Red.
Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TOSCI, Bw. Nyasebwa Chimagu, amesema TOSCI inaendelea kushirikiana na sekta binafsi pamoja na kuwawezesha wazalishaji wa ndani ili kuongeza uzalishaji wa mbegu nchini na kupunguza utegemezi wa mbegu zinazoagizwa kutoka nje ya nchi.

Amesema Serikali inaendelea kuweka msisitizo katika uzalishaji wa mazao ya bustani, hususan mboga mboga na viungo kama vitunguu, ambayo ni miongoni mwa mazao yanayotoa fursa za kiuchumi kwa vijana na wanawake nchini. Kwa mujibu wa Bw. Chimagu, kuongeza uzalishaji wa mbegu bora ndani ya nchi kutasaidia kuimarisha upatikanaji wa mbegu kwa wakulima na kuongeza tija katika kilimo.


Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here