Halmashauri ya Wilaya ya Nzega mkoani Tabora, imesajili vikundi 203 vikijumuisha wazee 11, wanawake 108, vijana 79 na watu wenye ulemavu watano.
Afisa maendeleo ya jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, AnnaMary Galibona ameeleza hayo mbele ya kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa mwaka 2026 Wazo Michael Mwang’onda akisoma taarifa ya usajili na ushiriki wa makundi maalumu kwenye mfumo wa ununuzi wa umma (PPRA).Galibona ameeleza kwamba hadi kufikia Septemba mwaka 2026 vikundi hivyo vimeshasajiliwa na Halmashauri hiyo na wana mikakati ya kuongeza zabuni kwa makundi maalum.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo










