Wanawake, Vijana, Wazee na Watu wenye mahitaji maalum wa mikoa ya Kanda ya Kusini wametakiwa kuchangamkia fursa zinazopatikana katika zabuni za Umma ili kuongeza ushiriki wao katika shughuli za kiuchumi na maendeleo ya taifa.
Wito huo umetolewa na Kaimu Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya Jamii Manispaa ya Lindi, Bi. Alusaria Mushi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Lindi, Mhe. Adam Malima katika Kongamano la Viwanda, Uwekezaji, Teknolojia na Uvumbuzi kwa Wanawake, Vijana, Wazee na Watu wenye mahitaji maalum wa mikoa ya Kanda ya Kusini lililoratibiwa na Chama cha Viziwi Tanzania (CHAVITA) jana mkoani Lindi.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo












