Tanzania imeendelea kujijengea heshima katika sekta ya mbegu barani Afrika baada ya Waziri wa Kilimo wa Jamhuri ya Sudani Kusini, Mhe. Clement Juma Mbugoniwia, kutembelea banda la Taasisi ya Kuthibiti Ubora wa Mbegu Tanzania (TOSCI) katika Maonesho ya Kitaifa ya Nanenane yanayoendelea Nzuguni, mkoani Dodoma, kujifunza mifumo ya kisasa inayotumika nchini kuhakikisha wakulima wanapata mbegu zenye ubora unaokidhi viwango vya kimataifa.
Ziara hiyo, iliyofanyika akiwa ameambatana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Bw. Gerald Mweli, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, ilitoa fursa kwa ujumbe huo kupata maelezo ya kina kuhusu hatua zinazochukuliwa na TOSCI katika kusimamia ubora wa mbegu kuanzia uzalishaji, uhakiki hadi usambazaji wake kwa wakulima, mfumo ambao umeendelea kuimarisha imani ya wakulima na wadau wa sekta ya kilimo nchini.Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TOSCI, Bw. Nyasebwa Chimagu, alisema taasisi hiyo ipo tayari kushirikiana na Serikali ya Sudani Kusini katika kujenga uwezo wa kitaalamu, kubadilishana uzoefu na kuimarisha mifumo ya udhibiti wa ubora wa mbegu ili kuongeza uzalishaji wa mazao na kukuza biashara ya mbegu bora ndani na nje ya mipaka ya nchi hizo.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo




























