Msigwa ataka kasi mradi wa uwanja wa michezo Dodoma

DODOMA-Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, amemtaka Mkandarasi wa mradi wa Uwanja wa Mpira Dodoma kuongeza kasi ili kuhakikisha kazi hiyo inakamilika kwa wakati kwa kuzingatia ubora na viwango vinavyohitajika.
Msigwa ametoa kauli hiyo Agosti 20, 2026 wakati akikagua maendeleo ya uwanja huo ambapo ameeleza hadi sasa uwanja huo umefikia asilimia 15.

Amesema kuwa, Serikali inaendelea kufuatilia kwa ukaribu ujenzi wa uwanja huo hadi utakapokamilika ili kuhakikisha unakidhi viwango vya kimataifa.
Aidha, Msigwa amewapongeza Wakandarasi na Wasimamizi wa uwanja huo kwa kazi nzuri, ambapo ameridhishwa na maendeleo yaliyofikiwa hadi sasa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here