SERIKALI imeonya kuwa mtu au taasisi itakayobainika kuharibu au kutenda kosa dhidi ya Miundombinu Muhimu ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (CII) atakabiliwa na adhabu kali kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya mwaka 2015.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angellah Kairuki, amesema hayo Jumatano Agosti 19, 2026 jijini Dar es Salaam ambapo ameeleza kuwa, kwa mujibu wa Kifungu cha 29 cha Sheria hiyo, mhusika anaweza kutozwa faini isiyopungua Shilingi milioni 100, au mara tatu ya hasara iliyosababishwa, au kifungo kisichopungua miaka mitano.
Amesema adhabu hizo zinaweza pia kutolewa kwa pamoja, ikiwemo faini na kifungo, kulingana na kosa lililofanyika dhidi ya CII.






Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo























