NA DIRAMAKINI
MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi amejiuzulu nafasi hiyo, huku Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt.Samia Suluhu Hassan akiridhia ombi hilo.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo, Jumanne, Agosti 25, 2026 na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt.Moses M.Kusiluka, Rais Samia amepokea barua ya ombi la kujiuzulu kutoka kwa Makamu wa Rais Nchimbi, akieleza kuwa anatarajia kuacha nafasi hiyo kuanzia Septemba 4, 2026.“Tarehe 25 Agosti, 2026 amepokea barua ya ombi la kujiuzulu Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi kuanzia tarehe 04 Septemba, 2026. Mheshimiwa Rais ameridhia ombi hilo,” imeeleza taarifa hiyo.
Kujiuzulu kwa Makamu wa Rais kunafungua hatua mpya ya mchakato wa kikatiba wa kujaza nafasi hiyo katika uongozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ofisi ya Katibu Mkuu Kiongozi imeeleza kuwa, taratibu za kikatiba za kumpata Makamu wa Rais mwingine wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania zitachukuliwa, bila kutoa maelezo zaidi kuhusu jina la atakayeteuliwa au muda wa uteuzi huo.
Kuondoka kwa Nchimbi katika nafasi ya Makamu wa Rais kuanzia Septemba 4 kunatarajiwa kuleta mabadiliko katika muundo wa uongozi wa juu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wakati taratibu za kikatiba za kumpata mrithi wake zikianza.
Tags
Breaking News
Dr Emmanuel John Nchimbi
Dr Emmanuel Nchimbi
Dr Samia Suluhu Hassan
Habari
Makamu wa Rais Ajiuzulu