Magazeti leo Agosti 22,2026

NAIBU Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu TAMISEMI, Bw. Atupele Mwambene ametoa wito kwa walimu walioshiriki mafunzo ya somo la Elimu ya Biashara kuonesha ushirikiano kwa walimu wataowakuta katika vituo vyao vya kazi ili kuwasaidia watoto katika malezi pamoja na ujifunzaji.
Ametoa wito huo Agosti 21, 2026 wakati akihitimisha mafunzo ya somo la Elimu ya Biashara kwa walimu wa kujitolea waliofadhliwa na Shirika lisilo la kiserikali la EDUCATE, tukio lililofanyika katika ukumbi wa Nkurumah chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Bw. Mwambene amesema, ili kufikia malengo ya kuboresha elimu katika mazingira mtayoenda msisite kuomba ushauri na miongozo ya kiutendaji kwa viongozi na wenyeji mtakaowakuta jambo litaloimarisha upendo na ushirikiano katika kutimiza wajibu wa malezi na ufundishaji kwa wanafunzi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here