Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) umeendelea kutoa mafunzo maalum ya siku mbili kuhusu Uongozi na Usimamizi wa Utekelezaji wa Mtaala Ulioboreshwa, yakilenga kuimarisha uwezo wa Wakuu wa Shule za Sekondari katika kusimamia kwa ufanisi mabadiliko ya mtaala.








Mafunzo hayo yameanza tarehe 24 na yatahitimishwa tarehe 25 Agosti 2026 katika Kampasi ya ADEM Bagamoyo, yamewashirikisha Wakuu wa Shule za Sekondari 163 kutoka Mkoa wa Ruvuma na yamefadhiliwa na Umoja wa Wakuu wa Shule za Sekondari Tanzania (TAHOSSA).
Katika mafunzo hayo, washiriki watajadili mada mbalimbali zinazolenga kuwajengea uwezo katika maeneo muhimu ya Uongozi na Usimamizi wa Shule, ikiwemo Uongozi na Usimamizi wa Shule, Usimamizi wa Utekelezaji wa Mtaala, Uchambuzi wa Mtaala Ulioboreshwa, Maadili na Itifaki pamoja na Huduma kwa Wateja.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo












