Wazazi na walezi wahimizwa kusikiliza, kutambua na kuwekeza katika vipaji vya watoto wao

DAR-Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mheshimiwa Hamis Mwinjuma, amewataka wazazi na walezi nchini kusikiliza, kutambua na kuwekeza katika vipaji vya watoto wao na kusisitiza kuwa jukumu la mzazi si kumchagulia mtoto atakachokuwa, bali kumsaidia kuwa bora katika kile anachoweza kufanya.
Amesema hayo Agosti 16, 2026 katika Mahafali ya 11 ya Darasa la Saba ya Shule ya Royal Elite, yaliyofanyika Mlimani City jijini Dar es salaam.

Mhe. Mwinjuma ameeleza kuwa kila mtoto ana uwezo au kipaji cha kipekee ambacho kinapaswa kutambuliwa na kuendelezwa ikiwa sambamba na elimu ya darasani.
"Mtoto akisema anapenda mpira, msimwambie moja kwa moja kwamba huo ni mchezo tu. Mtoto akisema anapenda kuimba, msimkatishe tamaa. Mtoto akionyesha kipaji cha sanaa, msaidieni kukiendeleza,”amesema Mhe. Mwinjuma.

Aidha, amesisitiza kuwa kulea kipaji hakumaanishi mtoto kuacha masomo, bali wazazi wanapaswa kumsaidia mtoto kuwa na elimu pamoja na kipaji, akieleza kuwa mtu anaweza kuwa msomi na wakati huo huo akawa Mwanamichezo,Msanii au Mbunifu.
Pamoja na mambo mengine, ametumia nafasi hiyo kuwasisitiza wazazi kuwa chanzo cha hamasa kwa watoto kwakuwa wakati mwingine mtoto huhitaji msaada mkubwa kutoka kwa mzazi zaidi ya kusikia akiaminishwa kuwa anaweza kufanikiwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here