Zingatieni sheria za usalama barabarani

KATAVI-Madereva wa bajaji mkoani Katavi wametakiwa kuzingatia sheria na kanuni za usalama barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kusababisha vifo,majeruhi na hasara za mali.
Hayo yamezungumzwa Agosti 13, 2026 na Sajenti wa Polisi Jojina Luoga kutoka Kikosi cha Usalama Barabarani wakati akitoa elimu ya usalama barabarani katika barabara kuu ya Mpanda-Kigoma kwa madereva hao huku akiwakumbusha kuacha tabia ya kuzidisha abiria maarufu kama “mshikaki” kitendo ambacho kinaweka maisha ya abiria na watumiaji wengine wa barabara katika hali ya hatari.
Aidha, Sajenti Luoga amewataka madereva bajaji kuacha mwendo kasi (over speed) na kuzingatia mwendo unaotakiwa kulingana na mazingira ya barabara pia wanapaswa kuwa mfano kwa kuzingatia sheria za usalama barabarani.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here