Bodi ya Wakurugenzi TRC yaridhishwa na utekelezaji Mradi wa SGR

MWANZA-Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) ikiongozana na Menejimenti imekamilisha ziara ya ukaguzi wa maendeleo ya ujenzi wa mradi wa Reli ya Kisasa (SGR) kuanzia Makutopora hadi Mwanza, na kueleza kuridhishwa na hatua kubwa iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi wa kimkakati wa Reli ya Kisasa (SGR).
Akitathmini matokeo ya ziara hiyo, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TRC Bw. Jaffer Machano ameeleza kuwa bodi imekagua maendeleo ya ujenzi kuanzia kipande cha tatu hadi kipande cha tano na kujiridhisha kuwa kazi inakwenda kulingana na mipango iliyowekwa.
Bw. Machano amesisitiza kuwa,matarajio ni kukamilika kwa mradi huo na treni ya SGR na kuanza uendeshaji ifikapo mwishoni mwa mwaka 2028 yapo kwenye mwelekeo sahihi na yanasadifu maelekezo ya Serikali.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here