Mashindano ya BAMATA kuchochea umoja wa majeshi nchini

MWANZA-Mashindano ya Baraza la Michezo ya Majeshi Tanzania (BAMATA) yanatarajiwa kuimarisha mshikamano, umoja na urafiki miongoni mwa vyombo vya ulinzi na usalama nchini, huku wananchi wakipata fursa ya kujifunza na kushuhudia michezo mbalimbali.
Mashindano hayo yatafanyika jijini Mwanza kuanzia Septemba 21 hadi Oktoba 5, 2026, katika Uwanja wa CCM Kirumba, yakiongozwa na kaulimbiu isemayo: “Tanzania ni yetu sote, tushikamane kwa pamoja kudumisha amani.”

​Akizungumza wakati wa maandalizi ya ufunguzi wa mashindano hayo, Mwenyekiti wa BAMATA, Meja Jenerali, Said Hamis Said, amesema michezo hiyo ni sehemu muhimu ya kuwaweka wanajeshi na watumishi wa vyombo vya ulinzi na usalama katika hali nzuri kiafya, pamoja na kuimarisha ushirikiano.
Michezo hiyo inashirikisha timu kutoka Kanda saba ambazo ni Kanda ya JKT, JWTZ, Ngome, Uhamiaji, SMZ, Jeshi la Zimamoto na Uokoaji pamoja na Jeshi la Polisi.

​Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, CP Salum Hamduni, amesema ushiriki wa vyombo hivyo katika mashindano hayo unaonyesha mshikamano na umoja uliopo kati ya vyombo vya ulinzi na usalama nchini.
Ameongeza kuwa, Mkoa wa Mwanza unajivunia kuwa mwenyeji wa mashindano hayo na kwamba wananchi wa mkoa huo wanatambua na kuthamini mchango mkubwa wa vyombo vya usalama katika kudumisha amani nchini.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here