Serikali imesema itaanzisha Kituo cha Forodha katika maeneo ya mpakani ya Tarafa za Loliondo na Sale, Mkoani Arusha, baada ya kukamilika kwa tathmini na endapo maeneo hayo yatakuwa yamekidhi vigezo vilivyowekwa.




Hayo yameelezwa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Ngorongoro, Mhe. Yannick Ndoinyo, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kujenga Kituo au Vituo vya Forodha katika maeneo ya mpakani ya Tarafa za Loliondo na Sale, Wilaya ya Ngorongoro.
Mhe. Munde alisema vigezo vinavyotumika katika kuanzisha vituo vya Forodha ni pamoja na hali halisi ya mpaka (strategic nature), idadi ya watu wanaoishi katika eneo husika la mpaka na kiasi cha mizigo kinachohudumiwa.
Tags
Kurasa za Magazeti
Kurasa za Mbele na Nyuma za Magazeti
Magazeti
Magazeti ya Leo
Magazetini
Magazetini leo
Yaliyojiri Magazetini Leo
















