Magazeti leo Septemba 6,2026

Serikali imesema itaanzisha Kituo cha Forodha katika maeneo ya mpakani ya Tarafa za Loliondo na Sale, Mkoani Arusha, baada ya kukamilika kwa tathmini na endapo maeneo hayo yatakuwa yamekidhi vigezo vilivyowekwa.
Hayo yameelezwa Bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb), alipokuwa akijibu swali la Mbunge wa Ngorongoro, Mhe. Yannick Ndoinyo, aliyetaka kujua mpango wa Serikali wa kujenga Kituo au Vituo vya Forodha katika maeneo ya mpakani ya Tarafa za Loliondo na Sale, Wilaya ya Ngorongoro.

Mhe. Munde alisema vigezo vinavyotumika katika kuanzisha vituo vya Forodha ni pamoja na hali halisi ya mpaka (strategic nature), idadi ya watu wanaoishi katika eneo husika la mpaka na kiasi cha mizigo kinachohudumiwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here