Rais Dkt.Mwinyi asisitiza umuhimu wa Madrasa katika kujenga kizazi chenye maadili mema nchini

ZANZIBAR-Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Alhaj Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesisitiza umuhimu wa madrasa katika kujenga kizazi chenye elimu ya dini, maadili mema na misingi imara ya malezi.
Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo Septemba 18, 2026 katika Dua Maalum ya kuliombea Taifa, viongozi wa nchi na kuomba kwa Mwenyezi Mungu kuiepusha Zanzibar na madhara yanayoweza kujitokeza kutokana na mvua kubwa pamoja na El Niño, iliyofanyika Almadrasat Swifat Nabawiyatil Karimah, Msolopa Kilimani, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Amesema ushirikiano kati ya walimu wa madrasa, wazazi, walezi, viongozi wa dini na jamii ni muhimu katika malezi ya watoto na vijana, hususan katika kipindi hiki cha matumizi makubwa ya teknolojia na mitandao ya kijamii.
Aidha, amewahimiza wananchi kuendelea kudumisha umoja, mshikamano na amani, pamoja na kuchukua tahadhari na kuzingatia taarifa na maelekezo yanayotolewa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania(TMA) na Serikali kuhusu mvua kubwa zinazotarajiwa.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here