Ubalozi wa Tanzania nchini Marekani watoa taarifa kuhusu kifo cha mwanadiaspora Khalifa H.Siwa

NA DIRAMAKINI

UBALOZI wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini Marekani umesema kwamba, upo kwenye mawasiliano na ndugu wa mwanadiaspora Khalifa H. Siwa aliyekuwa anaishi New Jersey na kufariki Septemba 2, 2026 jijini New York.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na ubalozi huo Septemba 4,2026 pia imefafanua kuwa, ubalozi unaendelea kushirikiana na ndugu wa marehemu pamoja na Jumuiya ya Watanzania wa New York (NYTC) katika kukamilisha taratibu za kusafirisha mwili wa marehemu kuja nchini Tanzania kwa ajili ya maziko.

"Tunaomba radhi kwa usumbufu wowote uliojitokeza na tunatoa pole nyingi kwa ndugu, jamaa, marafiki na wapendwa wote wa marehemu. Kwa mawasiliano tafadhali tuandikie kupitia barua pepe: ubalozi@tanzaniaembassy-us.org ," imeeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here