Zoezi la utwaaji ardhi mradi wa SGR kati ya Tabora na Kigoma linaendelea kwa kasi

KIGOMA-Shirika la Reli Tanzania (TRC) linaendelea na zoezi la utwaaji wa ardhi linaloambatana na uhamishaji wa makaburi katika Kipande cha Sita cha mradi wa ujenzi wa Reli ya Kisasa (SGR) kutoka Tabora hadi Kigoma linaloendelea kufanyika wilaya ya Uvinza, mkoani Kigoma.
Zoezi hilo linalenga kupisha maeneo mbalimbali ya ujenzi wa mradi huo wa kimkakati ili ikiwemo ujenzi wa njia kuu ya reli, madaraja na vivuko.

Mthamini kutoka TRC, Bw. Hassan Mbaga, ameeleza kuwa zoezi hilo la uhamishaji makaburi linagusa vijiji mbalimbali vikiwemo Nyangabo, Nguruka, Gweru, Malagarasi, Mpeta, vilivyopo katika wilaya ya Uvinza - Kigoma.
Katika kusaidia mchakato wa zoezi hilo, Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza, Bw. Hussein Katelanya , amebainisha kuwa zoezi la uhamishaji makaburi linafanyika kwa ushirikiano wa karibu kati ya TRC, Ofisi ya Mkurugenzi wa Wilaya, na Timu ya Huduma za Afya Kinga.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

Know matter how large or small your business is, advertising here