SIKIA HII! BODI YA UTALII TANZANIA YAJA NA MKAKATI KABAMBE WA KUWALETA WATALII

BODI ya Utalii Tanzania (TTB) imekutana na waandaaji wa kipindi cha televisheni kijulikanacho kama “Viumbe Hai” kinachorushwa na Azam TV kwa lengo la kupanga mikakati ya kushirikiana katika kutangaza utalii wa Tanzania ndani na nje ya nchi, inaripoti wwww.diramakini.co.tz
 

Kipindi hicho kinachorushwa mara nne kwa wiki, kwa msimu (season), kimejikita zaidi katika kuelimisha umma kuhusu tabia za wanyama mbalimbali wanaopatikana katika vivutio vya utalii vya Tanzania.

Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii nchini (TTB),Mindi Kasiga akisisitiza jambo mara baadaya ya kumaliza mkutano jijini Dar es Salaam Agosti 21, 2020.

Akizungumza wakati wa mkutano huo uliofanyika katika Ofisi za TTB jijini Dar es Salaam jana Agosti 21, 2020, Mkurugenzi wa Masoko TTB,Mindi Kasiga alisema, “ushirikiano baina ya TTB na Azam ni wa kimkakati kwa kuwa kwa pamoja tunatoa elimu kwa umma kuhusu utalii wa wanyama na viumbe hai.

"Viumbe Hai inatoa hamasa kwa watazamaji kujionea wanyama wakiwa katika maisha yao halisi na kusababisha idadi ya watalii wa ndani na nje kuongezeka,”alisema Mindi.

Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania (TTB),Mindi Kasiga akisikiliza kwa makini ujumbe unaotolewa na Mani Bakhresa wa Televisheni ya Azam wakati wa mkutano jijini Dar es Salaam Agosti 21, 2020.
 

Mwongozaji wa kipindi hicho,Mani Bakhresa alisema, Viumbe Hai kina watazamaji zaidi ya milioni tatu ndani na nje ya nchi na kuongeza kuwa ushirikiano na TTB umewezesha utayarishwaji wa Msimu wa Nne wa kipindi hicho kusheheni vivutio ambavyo Watanzania wengi hawajawahi kuviona.

“Watazamaji wetu wajiandae na msimu huu kuona tabia za Nyumbu wakivuka mto, Flamingo wa Ziwa Natron na Mbwa mwitu adimu sana kuonekana,”alisema Bakhresa.

Picha ya pamoja baina ya wajumbe wa mkutano wa Bodi ya Utalii nchini (TTB) na Televisheini ya Azam baada ya mkutano uliofanyika Agosti 21, 2020 jijini Dar es Salaam.
 

Msimu wa Nne wa Viumbe Hai unatarajiwa kuanza kuruka hewani pindi baada ya kukamilika utayarishwaji wa vipindi (episodes) vyote 12 vitakavyokamilisha msimu huo. 

Aidha, ili kuhamasisha na kutangaza utalii wa ndani, Bodi ya Utalii inakaribisha vyombo vingine vya habari kuibua vipindi kama ‘Viumbe Hai’ vitakavyotoa hamasa kwa umma na kujenga utamaduni wa kutalii na kutembelea vivutio
vya utalii vya Tanzania.

Baadhi ya wafanyakazi wa Bodi ya Utalii nchini (TTB) na Televisheni ya Azam wakiwa katika mazungumzo jijini Dar es Salaam Agosti 21, 2020.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news