WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene ameihakikishia Marekani kuwa, Tanzania ipo salama na itaendelea kuwa salama kwa raia wake na wageni mbalimbali waliopo na wanaoingia nchini,anaripoti MWANDISHI WETU kutoka MOHA.
Akizungumza na Balozi mpya wa Marekani Nchini, Dktt. Donald Wright, ofisini kwa Waziri huyo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, Waziri Simbachawene amesema usalama wa nchi upo juu na kwamba tumefanya vizuri katika kutambulisha wageni katika maeneo ya uwekezaji na utalii.
Pia Waziri Simbachawene alisema Serikali inaendelea kudhibiti biashara haramu ya binadamu ambapo mpaka sasa imeweza kuwarudisha Wasomali 1,300,000 wanaopita nchini kwenda Afrika Kusini.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (wapili kushoto), Balozi wa Marekani Nchini, Dkt. Donald Wright (katikati), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika, jijini Dodoma, leo. Simbachawene amemhakikishia Balozi huyo kuwa, Tanzania ipo salama na itaendelea kuwa salama kwa raia wake na wageni mbalimbali waliopo na wanaoingia nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto) akimuaga Balozi wa Marekani Nchini, Dkt. Donald Wright, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika, Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma, leo. Simbachawene amemhakikishia Balozi huyo kuwa, Tanzania ipo salama na itaendelea kuwa salama kwa raia wake na wageni mbalimbali waliopo na wanaoingia nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Pia Waziri Simbachawene alimemuhakikishia Balozi huyo kuwa, Serikali itaendelea kushirikiana na Marekani katika maeneo ambayo yana maslahi kwa Tanzania na Marekani.
Akizungumza na Balozi mpya wa Marekani Nchini, Dktt. Donald Wright, ofisini kwa Waziri huyo katika Mji wa Serikali Mtumba jijini Dodoma, Waziri Simbachawene amesema usalama wa nchi upo juu na kwamba tumefanya vizuri katika kutambulisha wageni katika maeneo ya uwekezaji na utalii.
Pia Waziri Simbachawene alisema Serikali inaendelea kudhibiti biashara haramu ya binadamu ambapo mpaka sasa imeweza kuwarudisha Wasomali 1,300,000 wanaopita nchini kwenda Afrika Kusini.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (wapili kushoto), Balozi wa Marekani Nchini, Dkt. Donald Wright (katikati), wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mazungumzo yao yaliyofanyika, jijini Dodoma, leo. Simbachawene amemhakikishia Balozi huyo kuwa, Tanzania ipo salama na itaendelea kuwa salama kwa raia wake na wageni mbalimbali waliopo na wanaoingia nchini. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
“Mafanikio haya ya kudhibiti biashara hii haramu ya binadamu ni
kutokana na kuwepo kwa sheria ya mwaka 2008 na kanuni zake ambapo
imeweza kutusaidia kudhibiti biashara hii kwa kutumia sheria za nchi,”amesema Simbachawene.
Ameongeza kuwa, mipaka ya nchi ipo imara
na Serikali inaendelea kuimarisha zaidi ambapo imeweza kudhibiti watu
wanaoingia na kutoka katika mipaka mbalimbali nchini.
Kwa upande
wake Balozi, Dkt. Wright ameipongeza Tanzania inavyoshughulikia biashara
haramu ya binadamu na alikiri hajawahi kukutana na kesi za ajabu
zinazohusiana na biashara hiyo.

Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene (kushoto) akimuaga Balozi wa Marekani Nchini, Dkt. Donald Wright, baada ya mazungumzo yao yaliyofanyika, Mji wa Serikali, Mtumba, jijini Dodoma, leo. Simbachawene amemhakikishia Balozi huyo kuwa, Tanzania ipo salama na itaendelea kuwa salama kwa raia wake na wageni mbalimbali waliopo na wanaoingia nchini. Picha zote na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi.
Pia Waziri Simbachawene alimemuhakikishia Balozi huyo kuwa, Serikali itaendelea kushirikiana na Marekani katika maeneo ambayo yana maslahi kwa Tanzania na Marekani.
Tags
Habari
