Naibu Kamishna wa Uhifadhi Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka
ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Imani Nkuwi amewataka
wafanyakazi wa mamlaka hiyo kufanya kazi kwa uzalendo, ueledi na kudumisha
upendo miongoni mwao ili kuiwezesha TAWA kufikia malengo yake yaliyokusudiwa, anaripoti Hassan Ninga (Diramakini) Tabora.
Nkuwi ametoa wito huo wakati akiwa katika ziara ya
kikazi mkoani Tabora na kufanya mazungumzo na watumishi wa vituo
vilivyopo chini ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) mkoani humo.
Naibu Kamishna wa Uhifadhi Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Imani Nkuwi alipowasili mkoani Tabora. (DIRAMAKINI).
Naibu Kamishna wa Uhifadhi Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Imani Nkuwi alipowasili mkoani Tabora. (DIRAMAKINI).Vituo hivyo ni pamoja na Kanda Dhidi ya
Ujangili ya Magharibi (KDU),Pori la Akiba la Ugalla,Pori la Akiba
Luganzo Tongwe na Pori la Akiba Wembere.
Katika ziara hiyo pamoja
mambo mengine, Naibu Kamishna Nkuwi alitoa ufafanuzi kwa watumishi hao
kuhusu mabadiliko mbalimbali yaliyofanywa na Serikali katika shirika
pamoja na kusikiliza changamoto zinazowakibili watumishi kwenye vituo
vyao.

Askari wa uhifadhi TAWA mkoani Tabora wakitoa heshima kwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Imani Nkuwi. (DIRAMAKINI).
Naibu Kamishna Nkuwi ametumia fursa kuwaasa watumishi
kuzingatia tunu za TAWA zilizoanishwa katika Mpango Mkakati wa TAWA
katika kutekeleza majukumu yao.
Aidha, amewaasa watumishi
kujiepusha na kushawishika kupokea rushwa katika utekelezaji wa majukumu
yao na kuhakikisha haki na sheria inafuatwa hasa wanapokamata majangili
na mifugo ndani ya hifadhi wanazosimamia.

Naibu Kamishna wa Uhifadhi Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Imani Nkuwi akisalimiana na wafanyakazi wa TAWA Tabora. (DIRAMAKINI).
Sanjari na
hilo ametoa ufafanuzi kwa watumishi kuhusu mabadiliko mbalimbali
yaliyofanywa na Serikali katika taasisi za uhifadhi zilizopo chini ya
Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kuboresha utendaji.
Ametaja baadhi ya mabadiliko hayo ni pamoja na Mabadiliko ya Kifungu cha 10 cha
Sheria Uhifadhi wa Wanyamapori Na. 5 ya mwaka 2009 kupitia sheria za
marekebisho mbalimbali Na. 02 ya mwaka 2020 ambayo imeanzisha rasmi
Jeshi la Uhifadhi wa Wanyamapori na Misitu (Wildlife and Forest
Conservation Service-WFCS). 

Naibu Kamishna wa Uhifadhi Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Imani Nkuwi akisaini kitabu cha wageni. (DIRAMAKINI).
Kufuatia mabadiliko hayo,
Wizara kwa kushirikiana na taasisi za uhifadhi inaandaa kanuni na
miongozo ya kutekeleza Sheria ya Jeshi la Uhifadhi.Hivyo, amewataka watumishi kubadilika kutoka mfumo wa kiraia na kuishi kwa kufuata taratibu za kijeshi.
Pia sheria imetoa baadhi ya mamlaka kwa watumishi ikiwepo ya kukamata,
kupeleleza, kufanya shughuli za kiintelijensia na kushughulikia mashauri
yanayohusisha mifugo kwa njia ya compound. 

Askari wa TAWA wakisimsikiliza, Naibu Kamishna wa Uhifadhi Utalii na Huduma za Biashara wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), Imani Nkuwi (hayupo pichani). (DIRAMAKINI).
Mengine ni mabadiliko ya
jukumu la kukusanya mapato ya Serikali ambalo limehamishwa kutoka
Taasisi za Uhifadhi (TAWA, TANAPA na NCAA) zilizo chini ya wizara kwenda
TRA kufuatia mabadiliko hayo taasisi husika zitakuwa zinapokea fedha za
kujiendesha kutoka Serikali Kuu.
Aidha,mabadiliko mengine
yamefanyika katika ngazi ya Wizara ni Uanzishwaji wa Idara ya Uratibu
wa Jeshi la Uhifadhi (paramilitary coordination division).
Kwa
upande wao watumishi wa TAWA mkoani Tabora walimweleza Naibu Kamishna
Nkuwi kuhusu changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo kwenye vituo
vyao vya kazi ambazo nyingi alizitolea ufafanuzi na maelekezo namna ya
kuzitatua ikiwa ni pamoja na kuandaa mapendekezo na mpango wa kina wa
biashara wa namna ya kuiboresha bustani ya wanyamapori ya Tabora ambayo
ipo katikati ya Manispaa ya Tabora.
Hata hivyo aliwapongeza
watumishi hao kwa kazi nzuri na ya kizalendo wanaoyoifanya ya kusimamia
raislimali ya wanyamapori kwa uaminifu kwa niaba ya watanzania.
Tags
Habari