FIFA yamfungia miaka mitano Rais wa Shirikisho la Soka Afrika

Bodi ya Uendeshaji Michezo ya Shirikisho la Soka la Kimataifa (FIFA) imemfungia miaka mitano Rais wa Shirikisho la Soka Afrika (CAF), Ahmad Ahmad kutojihusisha na mchezo wa soka na shughuli zote zonazohusiana na mchezo huo.
Kamati ya Nidhamu ya FIFA imesema Ahmad alikuwa na matumizi mabaya na ufujaji wa fedha za CAF akiwa madarakani. Rais huyo mwenye miaka 60 taarifa zinaeleza kuwa amekuwa kwenye uvunjifu wa taratibu zilizowekwa na kwenye masuala ya matumizi ya fedha kwa muda mrefu kwenye masuala ya fedha.

"Uchunguzi juu yake umefanywa kwa muda mrefu na ulianza baada ya kuingia madarakani mwaka 2017-2019, kuna mambo yalikuwa hayapo sawa kwenye masuala ya mipango na matumizi,"ilieleza taarifa ya Kamati hiyo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news