Rais Dkt. Mwinyi amuapisha Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia TEHAMA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi (katikati) akimuapisha, Rashid Said Rashid kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango anayeshuhulikia masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu jijini Zanzibar.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) akitia saini hati ya kiapo ya Rashid Said Rashid mara baada ya kumuapisha kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango anayeshuhulikia masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu jijini Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Hassan Mwinyi amemuapisha, Rashid Said Rashid kuwa Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, anaripoti Mwandishi Diramakini.

Hafla ya kuapishwa kiongozi huyo imefanyika leo Novemba 25, 2020 Ikulu jijini Zanzibar na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar Mhe.Zubeir Ali Maulid (kulia) Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar Dk.Mwinyi Talib Haji na Mkuu wa Wilaya ya Mjini pia Kaimu Mkuu wa Mkoa Mjini Magharibi Mhe.Marina Joel Thomas (kushoto) wakiwa katika hafla ya kuapishwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango anayeshuhulikia masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Rashid Said Rashid, iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar. 

Miongoni mwa viongozi hao ni Spika wa Baraza la Wawakilishi, Zubeir Ali Maulid, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Fedha na Mipango, Jamal Kassim Ali, Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar, Dkt. Mwinyi Talib Haji,  Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Abdulhamid Yahya Mzee na makatibu wakuu.  

Wengine ni Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar, Sheikh Hassan Othman Ngwali, Katibu wa Mufti Sheikh Khalid Ali Mfaume, Mkuu wa Wilaya ya Mjini, Marin Joel Thomas,wakuu wa vikosi vya ulinzi na usalama pamoja na viongozi wengine wa Serikali na wanafamilia. Wakuu wa Vikosi vya Ulinzi na Usalama Zanzibar wakiwa katika hafla ya kuapishwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango anayeshuhulikia masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Rashid Said Rashid, iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu Jijini Zanzibar. 

Katika maelezo yake mara baada ya kula kiapo Naibu Katibu Mkuu huyo ambaye pia atakuwa anashughulikia masuala ya fedha na kodi amesema kwamba, wananchi wana matumaini makubwa na mabadiliko kwani wanahitaji kupata huduma nzuri na zilizo bora zaidi.

Amesisitiza kwamba, teknolojia ya TEHAMA haitokuwa kwenye kodi pekee yake na badala yake itakwenda kwenye kila sekta ikiwemo uchumi wa buluu, huduma za afya, elimu na nyinginezo.

Aidha, amesema kuwa ipo haja ya kutumia teknolojia katika kutatua matatizo ya walimu na kusema kwamba Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) kina uwezo mkubwa wa kufanya hivyo, lakini kwa kuanzia alisema kuwa hatua hiyo itaanza katika ukusanyaji wa kodi kama alivyosisitiza Rais Dkt.Mwinyi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi (kushoto) akimkabidhi hati ya kiapo, Rashid Said Rashid mara baada ya kumuapisha kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango anayeshuhulikia masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika hafla iliyofanyika leo ukumbi wa Ikulu jijini Zanzibar.  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt.Hussein Ali Mwinyi (kulia) akiagana na Rashid Said Rashid mara baada ya kumuapisha kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango anayeshuhulikia masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) katika hafla iliyofanyika leo Novemba 24, 2020 katika Ukumbi wa Ikulu jijini Zanzibar. 

Amesema kwamba, lengo la Serikali ni kuhakikisha wananchi wanalipa kwa urahisi zaidi na kuepuka wananchi kwenda kulipa benki na kukaa muda mrefu, hivyo ni lazima mifumo ya awali iondolewe ikiwa ni pamoja na kupata wepesi katika kufuatia masuala ya vyeti vya kuzaliwa.

Ameongeza kwamba, Serikali itajipanga katika kuhakikisha wahitimu wa vyuo vya Zanzibar wanapata muelekeo kwa kuwatumia hapa hapa nchini na hakuna haja ya kuwaita wataalamu kutoka nje jambo ambalo litafanywa haraka iwezekenavyo ili kuondoa tatizo la walimu hasa wa sayansi.
Baadhi ya Viongozi waliohudhuria katika hafla ya kuapishwa kwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mipango anayeshuhulikia masuala ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA), Rashid Said Rashid (kutoka kushoto ni Waziri wa Fedha na Mipango, Jamal Kassim Ali,Katibu Mkuu wa Baraza la Mapinduzi ambaye pia ni Katibu Kiongozi, Dkt.Abduhamid Yahya Mzee,Naibu Kadhi Mkuu wa Zanzibar Sheikh Hassan Othman Ngwali na Katibu wa Mufti wa Zanzibar Sheikh Khalid Ali Mfaume. (Picha na Ikulu).

 Naibu Katibu Mkuu huyo alitangazwa siku ya Jumanne ya Novemba 22, 2020 ambapo Rais Dkt.Mwinyi alifanya uteuzi huo kwa mujibu wa kifungu cha 50(4) cha Katiba ya Zanzibar.

Kabla ya uteuzi huo Naibu Katibu Mkuu huyo alikuwa Mkurugenzi wa Mifumo ya Teknolojia ya Habari na Mawasilino (TEHAMA) katika Benki Kuu ya Tanzania, ambapo uteuzi wake ulianza rasmi Novemba 23, mwaka huu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news