Rais Magufuli ampangia aliyekuwa Mkurugenzi wa Jiji la Dar es Salaam Sipora Liana kuwa Mkurugenzi Manispaa ya Kinondoni

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt.John Pombe Joseph Magufuli amempangia kazi Bi.Sipora J. Liana kuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni kuanzia leo Februari 25, 2021, anaripoti Mwandishi Diramakini.

Taarifa iliyotolewa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe.Selemani Jafo imesema Bi. Sipora Liana amepangiwa majukumu hayo baada ya lililokuwa Jiji la Dar es salaam kuvunjwa hapo jana Februari 24,2021.
Bi.Sipora Liana

Waziri Jafo alieleza kuwa utaratibu wa kuwahamisha wafanyakazi katika vituo vingine utaendelea.

Aidha Waziri Jafo amemkabidhi Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es salaam Mhe.Omary Kumbilamoto (aliyekuwa Mstahiki Meya wa Ilala) Gari lililokua likitumiwa na Mstahiki Meya wa Jiji lililovunjwa la Dar es Salaam.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news