Waziri Ummy: Ajira za walimu 6,000 bado taratibu zikikamilika zitatangazwa

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Ummy Mwalimu amesema ajira za walimu 6,000 zitatangazwa hakuna kazi ambayo itatolewa kinyume na utaratibu,anaripoti Angela Msimbira (TANGA).
Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati akikagua ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule ya Sekondari ya Zingibari iliyopo kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.

Waziri Ummy amesema kuna matapeli wameibuka mitaani wakisema kuwa nafasi 6000 hazitatangazwa hivyo watumiwe fedha ili waweze kuwapangia vituo walimu wenye mahitaji na kazi hiyo, huo ni utapeli Serikali haitozi fedha kwa ajili ya ajira na haziwezi kutolewa kinyemela ajira hizo zikikamilika zitatangazwa.

Amewataka waalimu wanaokusudia kuomba nafasi hizo kuwa na subira mpaka zitakapotangazwa na Serikali itatenda haki kwa wote watakaokuwa wameomba nafasi hizo kwa kuzingatia sheria, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma.

Aidha,Waziri Ummy amesema kuwa Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Prof. Riziki Shemdoe ameanza kuchunguza kama matapeli hao ni watumishi wa Ofisi ya Rais-TAMISEMI au ni watu wa mitaani ambao wanadai fedha kwa watu kwa ahadi ya kutoa ajira na ikibainika hatua kali zitachukuliwa kwa mtumishi anayefanya vitendo vya utapeli huo.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news