Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na wananchi wa Kimamba wakati akitangaza maamuzi ya Rais Samia Suluhu Hassan kufuta mashamba 11 yenye ukubwa wa ekari 24,119 wilayani Kilosa mkoani Morogoro leo tarehe 7 Juni 2021.Uamuzi huo wa Rais Samia Suluhu Hassan unetangazwa leo tarehe 7 Juni 2021 wilayani Kilosa na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza kwa nyakati tofati na viongozi, watendaji na wananchi wa kijiji cha Kimamba wilayani Kilosa wakati wa ziara yake mkoani Morogoro.
Baadhi ya wananchi wa Kimamba wilayani Kilosa mkoa wa Morogoro wakimsikiliza Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi (hayupo pichani) wakati wa kutangaza kufutwa mashamba 11 yenye ukubwa wa ekari 24,119 wilayani Kilosa mkoani Morogoro tarehe 7 Juni 2021.Akielezea zaidi kuhusiana na mashamba 49 yenye ukubwa wa ekari 45,788.8 yaliyofufuliwa, Waziri Lukuvi alisema ekari 30,672.2 kati ya hizo lazima zirudi kwa wananchi na ekari 15,116.3 zilizobaki zipangiwe kwa ajili ya matumizi ya uwekezaji.
Kwa mujibu wa Lukuvi, wananchi watakaopewa mashamba ni wale wasiokuwa na ardhi kabisa na asingependa ardhi itolewe kwa watu wenye nia ya kujilimbikizia maeneo na kusisitiza anachotaka ni mashamba yasaidie wale wananchi wa kilosa kwa kujipatia kipato na kuinua maisha.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi akizungumza na viongozi wa wilaya ya Kilosa pamoja na watendaji wa vijiji vya Kimamba, Mvumi na Ilonga wakati akitangaza maamuzi ya Rais Samia Suluhu Hassan kufuta mashamba 11 yenye ukubwa wa ekari 24,119 wilayani Kilosa mkoani Morogoro leo tarehe 7 Juni 2021.Naye Mbunge wa jimbo la Kilosa ambaye pia ni Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi mbali na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa maamuzi aliyoyachukua kufuta mashamba 11 na kuridhia sehemu kutolewa kwa wananchi, alisema uamuzi uliofanywa na Rais unawagusa wana Kilosa hasa wana Kimamba na kuwataka kumuumga mkono kwa juhudi anazofanya kuwatumikia wananchi.
Baadhi ya mashamba yaliyofutwa ni pamoja na Sumagro Ltd lililopo Madoto na lenye ukubwa wa ekari 7,712, Bumagro Ltd Kivungu ekari 5660, M/S Sino Development (T) Ltd lililopo Kimamba ekari 6,945, Abdalah Islam lililopo eneo la Dodoma Isanga ekari 307, Mifugo Magairo la Magole lenye ukubwa wa ekari 489 na shamba la MS Masoni Company lililopo Magole ekari 466.
Mengine ni Mitibora (T) Ltd ekari 511 eneo la Magoli, Abdalah Islam ekari 307 Isanga Dodoma na Ibrahim Magairo mwenye shamba lenye ukubwa wa ekari 516 lililopo eneo la Magole.
Katika mwaka wa fedha 2020/2021 jumla ya mashamba 123 yalihakikiwa katika wilaya za Kilosa, Mvomero na Morogoro DC na kati yake mashamba 11 yenye ukubwa wa ekari 24,119 yalibatilishwa na Mhe. Rais kutokana wamiliki wake kukiuka taratibu za uendelezaji.