RC wa Geita atangaza jambo kubwa litakalotokea kesho asubuhi

NA MWANDISHI DIRAMAKINI

Mkuu wa mkoa wa Geita, Rosemary Staki Senyamule ametangaza rasmi usiku huu kuwa, kesho saa tatu asubuhi ataongoza wananchi wote wa Geita kwenda kuchangia damu katika banda la Waandishi wa Habari wa mji wa Geita (GMG) ,lengo likiwa ni kuokoa maisha ya wanawake wanaopungukiwa damu wakati wanajifungua na wanaopata ajali hasa bodaboda.
Mkuu wa Mkoa wa Geita, Rosemary Senyamule (katikati),Makamu Mwenyekiti wa GMG,Mutta Robert (kulia) na Magdalena Gumbu Mtaalam kutoka kitengo cha damu salama Hospitali ya Mkoa wa Geita (kushoto).
"Mimi Rosemary Staki Senyamule, Mkuu wa Mkoa wa Geita. Keshosho tarehe 25/09/2021 nategemea kwenda kutoa damu ili kuokoa maisha ya wanawake wanaopungukiwa damu wakati wa kujifungua pamoja na watu wanaohitaji damu kwa kupata ajali wakiwemo bodaboda.

"Nakuomba uniunge mkono ili tuokoe maisha. Hatujui na sisi tutahitaji damu lini na nani atatuokoa. Mhali ni eneo la maonesho EPZ Bombambili na muda ni kuanzia saa 3.00 hadi saa 11.00 jioni. GEITA YA DHAHABU, UTAJIRI NA HESHIMA. Karibu tuupe Heshima Mkoa wetu,"ameeleza usiku huu.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news