Bernard Membe atua mahakamani kusubiri huku dhidi Cyprian Musiba

NA MWANDISHI MAALUM

Aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje, Bernard Membe amefika katika Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda Maalum ya Dar es Salaam leo kwa ajili ya kusubiri hukumu dhidi ya Cyprian Musiba.
Hukumu hiyo ni ya shauri la kesi namba 220 ya mwaka 2018 ambapo kesi hiyo iliitwa kwa mara ya kwanza Februari 26, 2019.

Katika kesi hiyo Membe amemshtaki Musiba, Mhariri wa gazeti la Tanzanite na Wachapishaji wa gazeti hilo ambapo anawadai Tsh. Bilioni 10 kwa kumchafua, hukumu hiyo inatarajiwa kutolewa mbele ya Jaji Joacquine De Melo.

Musiba katika kesi hiyo anashtakiwa kwa kumtuhumu Membe kuwa anamhujumu Rais John Magufuli asitekeleze majukumu yake ya kuwaletea wananchi maendeleo huku akidai kwamba mbinu mojawapo ya kukamilisha hujuma hizo ni maandalizi anayofanya kugombea urais mwaka 2020 kupitia CCM.

Mheshimiwa Bernard Membe alikuwa miongoni mwa wagombea Urais katika Uchaguzi Mkuu 2015.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news