Manchester United yajiandaa kuachia kichapo kwa Watford

NA MWANDISHI MAALUM

KOCHA wa Manchester United, Ole Gunnar Solskjaer amesema mashabiki wa timu hiyo wataona mabadiliko kiuchezaji kwenye timu hiyo kuanzia kwenye mechi ya leo Jumamosi Novemba 20,2021 dhidi ya Watford.
Ole Gunnar Solskjaer amesema hayo baada ya kikosi hicho kupitia wakati mgumu wa matokeo ikiwa inashika nafasi ya sita kwenye msimamo katika mechi 12.

Baada ya mapumziko ya mechi za kimataifa, kocha huyo anasema, kila mmoja anaonekana mwenye ari kubwa.

“Wachezaji, viongozi, mimi mwenyewe na klabu inafanya kazi kwa ushirikiano kuhakikisha tunarudi kwenye njia zetu za ushindi,"amesema.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news