Wahabeshi 234 wafikishwa mahakamani mkoani Tanga

NA HADIJA BAGASHA

IDARA ya Uhamiaji mkoani Tanga imewafikisha mahakamani wahamiaji haramu wapatao 234 raia wa Ethiopia walioingia nchini kinyume cha sheria kwa nyakati tofauti kuanzia Septemba mwaka huu huku wengine 600 wakiwa katika Gereza Kuu la Maweni.
Sanjari na wahamiaji hao kukamatwa na kufikishwa mahakamani, wengine zaidi ya 600 wapo katika gereza Kuu la Maweni mkoani Tanga, wakitumikia vifungo na wengine wakisubiri mashauri ya kesi zao zilizopo mahakamani.
Kamanda wa Idara ya Uhamiaji mkoani Tanga, Petro Malima amesema kuwa, wahamiaji hao baada ya kukamatwa hawakuwapeleka mahakamani kutokana na kukosekana kwa mkalimani wa lugha wanayoongea ambayo ni Amalek inayozungumzwa na Wahabeshi hao.

Amesema, katika wahamiaji hao wapo pia Watanzania tisa ambao walikutwa wakiwasafirisha kwa kutumia usafiri wa pikipiki tano ambazo zinashikiliwa na idara hiyo na endapo watatiwa hatiani na mahakama, pikipiki hizo zitataifishwa na serikali.

Kamanda huyo amesema, wahamiaji hao wamefikishwa mahakamani nusu yao na wengine watafikishwa siku inayofuatwa kutokana na idadi yao kubwa.

Amesema, kwa upande wa Watanzania endapo watapatikana na makosa adhabu yao ni kifungo cha miaka 20 jela au kulipa faini ya shilingi milioni 20 au vyote kwa pamoja.
Kutokana na hali hiyo, Kamanda huyo wa Uhamiaji aliwataka wananchi washirikiane kuwabaini watu wanaoingia nchi kinyume cha sheria kwa kuwa hawajulikani kama wanapoingia ni makosa gani ya kisheria wanaweza kufanya lakini pia aliwaonya wale wanaojihusisha na biashara ya kuwasdafirisha waache mara moja.
Amesema, Serikali inatumia gharama kubwa kuwatunza endapo wataingia nchini hivyo ni vema wananchi wakawa walinzi ili kuokoa gharama hizo ambapo endapo serikali itawarejesha nyumbani kwao nauli kwa mhamiaji mmoja ni kuanzia dola 700 hadi 1,500.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news