Rais Samia ateua Mwenyekiti Tume ya Uchaguzi, viongozi mbalimbali

NA GODFREY NNKO

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali akiwemo Jaji Jacob Casthom Mwambegele aliyeteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).

Jaji Mwambegele anachukua nafasi ya Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani Semistocles Kaijage ambaye amemaliza muda wake.
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Jaffar Haniu amethibitisha hayo kupitia taarifa aliyoitoa leo Desemba 27,2021.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo,pia Rais amemteua Jaji Mwanaisha Athuman Kwariko kuwa mjumbe wa tume hiyo.

Jaji Kwariko anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Jacob Casthom Mwambegele.

Mheshimiwa Rais Samia pia amemteua Jaji Sam Mpaya Rumanyika, kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani.

Taarifa hiyo imeeleza pia Rais amemteua Profesa Khamis Dihenga kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB). Kabla ya uteuzi huo Profesa Dihenga alikuwa anahudumu kwa Mkataba katika Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA), Morogoro. 

Profesa Dihenga anachukua nafasi ya Profesa William Anangisye aliyemaliza muda wake.

Rais Samia pia amemteua Mhadhiri Mwandamizi, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dkt Mussa Muhidin Kissaka, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Serikali Mtandao (eGA) ambapo uteuzi huo umeanza Desemba 23, 202.1

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news