NA MWANDISHI DIRAMAKINI
MAKAMU wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mhe. Othman Masoud Othman, leo Januari 31, amefika na kutoa mkono wa pole kwa Familia ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt.Hussein Ali Mwinyi, kufuatia kifo cha Shangazi yake Bi.Hamisa Hassan Mwinyi, aliyefariki na kuzikwa leo huko Yombo jijini Dar es Salaam.
Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Januari 31, 2022 na Kitengo cha Habari Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar.
Marehemu Bi.Hamisa alizaliwa mwaka 1946 na hadi anafariki alikuwa na umri wa miaka 76. Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya marehemu. Amen.