Waziri Mchengerwa atoa maelekezo kwa watumishi wa wizara yake

NA MWANDISHI MAALUM

WAZIRI wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe, Mohamed Mchengerwa amewataka watendaji wote wa wizara yake kujitafakari utendaji wao na kufanya kazi kwa kuzingatia weledi ili kuendelea kuleta mapinduzi makubwa kwenye Sekta ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Waziri Mchengerwa ameyasema haya wakati alipokuwa akifungua kikao cha kupitishwa kuhusu maandalizi ya Bajeti na Randama kwa mwaka wa fedha 2022/23 na kamati ya bajeti leo Machi 20, 2022 katika ukumbi wa MAELEZO jijini Dodoma.

"Naomba niwatake watendaji wote kufanya kazi kwa kufuata maadili na taratibu za kazi za Serikali ili kuleta mafanikio kwa wananchi kwa ujumla,"amefafanua Mhe. Mchengerwa.

Amewataka Wakuu wa Idara wote kuwa na vikao vya kiutendaji na watumishi wao ili kuleta mageuzi ya kiutendaji na kuwataka watendaji kufanya kazi kama timu moja huku wakifungua milango ya wadau kama wasanii ili kujua haki zao.

“Watendaji tokeni waelezeni wasanii ili waweze kujisajili ili waweze kupata haki zao na wapate manufaa,”amesema.

Kwa upande mwingine, Mhe. Mchengerwa amesema Wizara imefanya mambo makubwa kwenye sekta za michezo, sanaa na Utamaduni na kwamba kinachotakiwa sasa ni kuendelea kufanya vizuri.
Ametumia tukio hilo kumshukuru Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe.Samia Suluhu Hassan kusaidia sekta za Utamaduni, Sanaa na Michezo katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali yake.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news