Waziri Mhagama:Serikali ya Awamu ya Sita imefanya mambo makubwa

NA JAMES K.MWANAMYOTO

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama amesema Serikali ya Awamu ya Sita katika kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa Mhe. Samia Suluhu Hassan imefanikiwa kuzingatia maslahi ya Watumishi wa Umma hivyo kujenga morali ya kiutendaji kwa watumishi hao.
Mhe. Jenista amesema hayo leo jijini Dodoma wakati wa mkutano wake na vyombo vya habari uliolenga kuuhabarisha umma kuhusu mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.

Mhe. Jenista amesema katika kipindi cha mwaka mmoja, Serikali imesimamia mageuzi makubwa kwenye Utumishi wa Umma katika kutazama maslahi ya watumishi, ikiwemo suala la upandishaji madaraja ambapo imewapandisha madaraja Watumishi wa Umma 190,781 wenye sifa stahiki na katika zoezi hilo jumla ya shilingi bilioni 39,649,988, 204 zimetumika.

Mhe. Jenista ameongeza kuwa Serikali imelipa madeni ya mishahara ya Watumishi wa Umma 65,394 yenye thamani ya shilingi bilioni 91,087,826,006.34 ambayo walikuwa wakidai kwa muda mrefu.

Sanjali na hilo, Mhe. Jenista amesema, Serikali imetumia shilingi bilioni 1,330,306,572 kwa ajili ya kuwabadilisha kada na kuwalipa mishahara Watumishi wa Umma 19,386.

Katika kuboresha huduma kwa wananchi, Mhe. Jenista amesema, Serikali imeongeza rasilimaliwatu kwa kutoa vibali vya ajira mpya na mbadala12,336 vilivyogharimu jumla ya shilingi bilioni 7,761,869,809.
Sehemu ya Watendaji wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Waandishi wa Habari wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza kwenye mkutano wake na Waandishi wa Habari uliolenga kuuhabarisha umma kuhusu mafanikio ya Serikali ya Awamu ya Sita katika kipindi cha mwaka mmoja cha uongozi wa Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Mhe. Jenista amesema, Serikali ya Awamu ya Sita imewapunguzia Watumishi wa Umma asilimia moja (1%) ya makato ya PAYE kutoka asilimia 9 hadi asilimia 8 lengo likiwa ni kuwapunguzia watumishi mzigo mkubwa wa kodi hivyo kuwaongeza kiwango cha mshahara kinachobakia (Net salary) kutokana na kupungua kwa kodi ya PAYE.

Hatua ya Serikali ya Awamu ya Sita kuzingatia maslahi ya Watumishi wa Umma kumewawezesha Watumishi wa Umma kuwa na morali ya utendaji kazi yenye tija katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi.

Diramakini

DIRAMAKINI is Tanzanian news media house established to play role in shaping the global agenda through telling true stories by delivering quick and in-depth.Our readers trust our coverage of the issues that matter most to them. Our agenda-setting journalism attracts. Contact us on diramakini@gmail.com OR +255 719 254 464.

Post a Comment

Previous Post Next Post

International news